Kwa mujibu wa Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza, Abu Alaa Al-Wala’i, katika ujumbe wake wa hamasa uliochapishwa kwenye mtandao wa X katika siku za kuelekea kutangazwa kwa makubaliano kati ya Tehran na Washington, alizungumzia nafasi ya juu ya ustahimilivu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mbele ya maadui wake na kusema: “Leo tupo katikati ya tukio kubwa la kihistoria. Muqawama wa Kiislamu wa Iraq, kupitia juhudi na mapambano yake katika njia ngumu ya Dhāt ash-Shawkah, umeandika ukurasa wenye kung'ara katika ushindi huu na umeweka mchango wake kwa herufi za nuru katika historia ya heshima ya Umma wa Kiislamu.”
Alieleza kwamba; irada ya chuma ya mujahaidina ndiyo iliyokuwa sababu kuu ya kuvuka vikwazo vigumu zaidi, na akaongeza: “Subira na ustahimilivu wa wapiganaji hatimaye vimezaa matunda, na kwa kufikiwa kwa malengo makubwa, Ahadi ya Kweli imetimia.”
Katibu Mkuu wa Kataib Sayyid al-Shuhadaa (as), akiendelea na hotuba yake huku akifanya upya ahadi kwa makamanda mashahidi wa muqawama, alisisitiza: “Tukimuelekea shahidi mtukufu Imam Khamenei, na lulu ya Lebanon shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, pamoja na mashahidi wote wa njia hii yenye baraka, tunatangaza kwamba; bado tumesimama imara juu ya njia ileile; na katika msamiati wetu hakuna hata chembe ya kurudi nyuma wala kufanya maridhiano.”
Mwishoni, Al-Wala’i alihitimisha ujumbe wake kwa kauli ileile ya ushindi:
«فُزنا وربّ الكعبة»
“Naapa kwa Mola wa Al-Kaaba kwamba tumefaulu na tumepata ushindi.”

Maoni yako